Pages

Sunday, December 29, 2013

ANGALIA JINSI MWAKA 2013 ULIVYO KUWA WA MAFANIKIO KWA CHADEMA.
  
KANDA NA CHADEMA NI MSINGI

Baada ya kuundwa kwa kanda ambayo ni mmoja ya mafanikio ya mwaka, ilianzishwa program ya Chadema ni msingi. Kwa ufupi hii ni program ya ujenzi wa chama ngazi ya kitongoji ambapo msingi mmoja unakuwa na viongozi na wanachama wasiopungua 30.

Ktk kikao cha Kanda ya ziwa magharibi hivi karibuni, taarifa iliyotolewa ni kuwa asilimia 48 ya vitongoji vya kana hiyo tayari ina misingi ya chama. Haya ni mafaniko makubwa sana kufanyika kwa mwaka mmoja. Na kwa kuwa program hii inaendealea mpaka Feb 20 . 2014 inawezekana kufikia 60%.

Kinachotia moyo zaidi ni kuwa program hii imefanyika huku wapinzani wetu Ccm wakiwa busy kutuchonganisha makao makuu. Nadhani hawakupima madhara ya kanda au labda mfumo wao wa ku-ditect hatari ni dhaifu. Tunasubiri taarifa rasmi ya kanda nyingine kupima mafanikio haya.

MABARAZA YA KATIBA MPYA:-

Kwa kutumia kanda chama kilisambaza fomu maalum majimbo yote nchini ili wanachama wetu watoe maoni yao kwa mchakato mpya. Kwenye jimbo naloishi mimi kwa mfano wanachama 11180 walijaza fomu hizo. Haya ni mafanikio ya kujivunia maana chama kiliwashirikisha katika suala kubwa la kitaifa.

Baada ya kujazwa kwa fomu hizo, chama kikaja na mbinu nyingine ya kukusanya maoni. Kikanyanyua Chopper mbili, moja na Dr Slaa na Marando na nyingine chini ya Kamanda Mbowe, Lissu na Mnyika. Ikapigwa mikutano nchi nzima watu wakajaa kwa maelfu (Chama kikatangazwa..
?)

Huko bungeni nako moto ukazidi kuwaka, mara mbili wabunge wakatoka nje ya bunge kushinikiza mambo wanayotaka katika sheria ya mabadiliko ya katiba. Mara mbili wakatinga Ikulu na rais akakubaliana na mapendekezo yao. Watanzania wakatambua ni chama gani kinataka katiba bora.

HATUA ZA KINIDHAMU NDANI YA CHAMA:-

Aliyekuwa makamu mwenyekiti Bavicha Juliana Shonza na wenzake walifukuzwa uanachama, huku naibu katibu mkuu Zitto Kabwe na wenzake wakivuliwa nyadhifa zao. Wengi wanalichambua suala hili ktk sura ya mgogoro lakini lina faida zake.

Kwanza limeonyesha ni chama makini kisichomwopa mtu bila kujali nafasi na umaarufu wake. Lakini kosa la Ccm kuwapokea Shonza na wenzake kulithibisha madai kuwa vurugu zinzoendelea kwenye chama chetu zinafadhiliwa na Ccm.

SUALA LA RWAKATARE NA UGAIDI:-

Itakumbukwa kuwa mwaka huu ndo tumeshuhudia mkurugenzi wetu wa usalama akibambikizwa kesi mbaya ya ugaidi. Pamoja na kiongozi mkubwa ndani ya chama kushauri Rwaks atoswe na chama sijui kwa faida gani, chama kiliamua kufa naye (shukrani kwa wanasheria wetu mahiri) Rwaks akashinda kesi na hira za wabaya zikashindwa.

Wabaya wetu hawakukata tamaa, sasa wakaona liwalo na liwe! Wakaona wammalize mwenyekiti na Lema. Wakarusha bomu kwenye mkutano pale Soweto (Chama kina ushaidi na Mkuu wa kaya). Lakini Mungu ni mwema mwenyekiti wetu na Kamanda Lema wote wakaokoka ingawa makanda wengine watoto kwa wakubwa walipoteza maisha.

Damu yao itaandika historia ya ukombozi wa mara ya pili ambayo tunapambana na ndugu zetu ambao ni wabaya kuliko wageni waliotutawala wakati huo wa ukolo ni. Lakini upande wa pili wa uzuri wa shambulizi hili, limetufundisha kwamba vita hii si lelemama bali ni mapambano kamili ya kuikomboa nchi yetu na kupigania chama chetu.

Yote haya kwangu ni mafanikio makubwa, misusuko yote tuliyopata tumeweza kupita ktk mwaka huu kwa mafanikio makubwa. Katika mwaka unaofuata mapambano yatakuwa makali zaidi maana ni mwaka wa uchaguzi serikali za mitaa, uchaguzi ndani ya chama na kupitisha katiba mpya.

Tunahitaji uongozi imara usiyoyumba utakaotuvusha katika haya na kuikomboa nchi yetu mwaka 2015. Niliwahi kuandika huko nyuma humu, kwama hatuwezi kubadali kocha timu inafanya vizuri. Tufanye marekebisho madogo kwenye safu alafu tusonge mbele. 

Nawasilisha! 

CHADEMA CHAMA CHETU, TANZANIA NCHI YETU.

Wednesday, December 25, 2013

USHAURI KWA VIJANA WA KITANZANIA

Hakuna mtu asiyependa utajiri lakini utajiri unaweza kupatikana bila kufanya biashara haramu au kujihusisha na mambo ya kuhatarisha maisha yako. Kwa miaka ya karibuni kumekuwa na Watanzania wengi wanajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya na wanaofaidika ni wachache tu wengi wao wanaishia kupata pesa ndogo na wanahatarisha maisha yao kwa kufugwa, kifungo cha kifo na hata madawa kupasuka tumboni na kuwaua. Kabla hujapata utajiri wa kudumu unatakiwa kupenda maendeleo kwanza na sio sifa pekee kwenye jamii. Fanya yafuatayo na polepole utafanikiwa.

1. Tafuta mtu ambaye unataka kuwa kama yeye: Usiangalie ukabila udini wala rangi ya mtu. Kama unataka kuwa kama Mengi, Mkono, Manji, Wanasiasa, wasomi au hata wasomi wa kimataifa wanaofanya kazi kwenye UN, World bank, diasporas. Tafuta mtu mmoja au wawili na waombe wawe kama walimu wako. Usiogope kutafuta utapata mtu na fuata wanayo kuambia hata kama wewe huoni umuhimu kwa sasa.

2. Jiendeleze kielimu: Hakuna mtu ambaye hawezi kufanya hili hata kama ni polepole. Elimu sio lazima iwe ya degree kwani duniani sasa kazi zinazolipa hazifundishwi kwenye degree bali certification mfano sasa tuna gas jifunze ufundi wa machine za kuchimba mafuta, project management, computer language, database kama SAP,Oracle, dot.net. Vilevile kuna Veta tafuta kitu ambacho kinauhusiano na Gas na Oil. Kwa ujumla jiwekee utamaduni wa kujiendeleza.

3. Marafiki: Tafuta marafiki ambao wanakusaidia kujiendeleza na wanakupenda badala ya wale wanaotaka kukutumia na wanao ku support kinafiki. Kama huna marafiki wazuri tafuta uhusiano wa kuomba kama mtanzania mwenzako omba urafiki kama Watanzania walivyokuwa wanafanya miaka ya zamani. Marafiki wabaya watakupeleka jela na kukuingiza kwenye ushabiki wa kimaisha na kukutumia.

4. Acha kulalamika: Kama unataka kuendelea uache utamaduni wa kulalamika badala yake jiulize je ni kitu gani naweza kufanya kufanikiwa bila kuiba. Tabia nzuri inaweza kukupeleka mbali kuliko unavyofikiri pesa pekee sio sababu ya kushidwa kuanza bali mara nyingi ni tabia. Ukiwa na tabia nzuri na kujihusisha na watu wazuri pesa haitakuwa kigezo.

5. Nenda ugaibuni kama umeshidwa yote: Kama yote umeshidwa na mazingira uliyo nayo si mazuri labda kabla ya kujihusisha na biashara haramu jitoe kwenye mazingira uliyopo. Kama bado ni kijana na mambo hayaendi yote hapo juu tafuta njia za kwenda nje lakini hayo mambo hapo juu inabidi uyafuate hata kama uko ugaibuni.

6. Uvumilivu: Hii nitakupa mfano wa ukweli kabisa. Watanzania wengi tulikuwa USA miaka ya 1996-2000 kutafuta maisha kwenda shule n.k. Watanzania wote tuliishi pamoja na mimi nilikuwa mojawapo pale Houston, TX tulifanya kazi pamoja umri ulikwa kama sawa tu kwa ufupi tulianza wote kwenye zero. Baaada ya miaka michache Watanzania wengine walihusisha na biashara, wengine shule, wengine mission town deals. Waliopiga deal walichukua pesa na kukimbia Tanzania na hawa walienda na magari, pesa na walipata wanawake, wanaume wanaowataka nyumbani. Wengi wao walienda bila kumaliza shule au kujifunza biashara.